Kiongozi wa kundi maarufu la Nyimbo
za Asili la Makhirikhiri la nchini
Botswana, Mosesi Malapela a.k.a
Shumba Ratshega, ametangaza kumrudia
Mungu baada ya kuokoka na kuanza
kuhubiri neno la wokovu.
Habari za uhakika kutoka kwa Msemaji
wa Kundi la Makhirikhiri Tanzania,
Livingstone Mkoi zilieleza kuwa, kwa
sasa kiongozi huyo amezaliwa upya
baada ya kuachana na kila kitu cha
kidunia na kuamua kumtumikia Mungu
katika maisha yake.
Livingstone alifunguka: “Ni kweli
Shumba amenieleza kuwa niwaambie
Watanzania kuwa anawaheshimu na
kuwakumbuka kutokana na mapokezi
makubwa waliyompa mwaka 2010
alipofika Tanzania kufanya matamasha
yake yaliyoandaliwa na Kituo cha Radio
Times FM na kumpa mafanikio
makubwa.
“Shumba anasema kuwa katika maisha
yake mapya ya utumishi wa Mungu
amekuwa akiiombea sana Tanzania
pamoja na Rais Dk. John Pombe
Magufuli.
“Kuhusu kuimba anasema ataendelea
kuimba tu na kundi lake halitakufa kwa
vile ule ni utamaduni wao wa asili.”
Mkoi aliongeza: “Tayari mtumishi huyo
ameanza ujenzi wa kanisa lake kubwa
kwenye mji mkuu wa nchi hiyo
(Gaborone) kwa ajili ya kuhubiri Neno la
Mungu.
Wednesday, April 26, 2017
11:35 AM
Unknown
News
No comments
Related Posts:
YAMETIMIA MADAM FROLA MBASHA KUFANYA BONGE LA HARUSI NA ATAZINDUA ALBAM NA KITABU CHA SIRI ZAKE Hayawi Hayawi sasa yamekuwa,lile tukio kubwa kabisa lililokuwa likisubiriwa kwa hamu na wengihatimaye siku imewadia.Si kingine bali ni harusi ya mwimbaji mahiri wanyimbo za injili kutoka nchini Tanzaniaanayefahamika k… Read More
HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO TAREHE 11 APRIL 2017 |V.I.TZ … Read More
V.I.TZ | HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO 12/4/2017 BOFYA HAPA KUTAZAMAGood Morning my people, today is 12 April 2017 and as usual my daily morning I give big news on the pages of newspapers from the Beginning and End of the Retort, Hardnews and Sports to find out what is going on my man do not … Read More
UDOM: MUSA MPUME KUZINDUA ALBAM YAKE 23/4/2017 | V.I.TZIn habari njema zenye furaha teleee KIJANA WA UDOM MUSA MPUME (DAKTARI MWIMBAJI) anatarajia kufanya uzinduzi WA Album yake ya kwanza tarehe 23/4/2017 jumapili Mahali tukio litakapofanyika ni CHUO KIKUU CHA DODOMA(UDOM) K… Read More
MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI AMANI MWASOTE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA NJE Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, imemuhukumu kifungo cha nje cha miezi sita na kulipa faini ya Sh1 milioni, Aman Mwasote baada ya kutiwa hatiani kwa kumwita mtoto wa miaka tisa kuwa mchawi. Mwasote, ambaye ni mwimbaji … Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment