Sunday, February 19, 2017

Lori lililogangana na gari dogo lenye
namba za usajili T353 DGE na
kusababisha Vifo vya watu kadhaa
TANZIA: Ajali mbaya iliyotokea usiku wa
kuamkia leo maeneo ya Mikese,Morogoro
yapelekea kufariki kwa mmliki wa Hoteli
iitwayo Villa Park iliyopo Mji mdogo wa
Makambako, Wilaya ya Njombe Mkoani
Njombe.
Mfanyabiashara huyo amefariki papo
hapo akiwa na mpenzi wake ambaye
hajajulikana kutokana na mwili wake
kuharibika vibaya sana kwa ajali.
Bw.Kizito siku ya jana alianza safari
akitokea Mji wa Mafinga kuelekea Jijini
Dar es Salaam baada ya kumalizika
mechi ya mpira wa miguu kati ya Njombe
Mji ya Mjini Njombe na Kurugenzi ya
Mjini Mafinga ambapo alienda
kuishangilia Timu yake ya Njombe Mji
iliyoibuka kidedea kwa kuichapa mabao
2-0 Timu ya Kurugenzi na kufanikiwa
kukata tiketi ya kushiriki Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania kuanzia msimu ujao
wa 2017/2018 .

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Popular Posts

Our Facebook Page

Video