Sunday, January 29, 2017

Mtu mmoja amekufa na wengine wanne kujeruhiwa mjini Tukuyu wilayani hapa, baada ya radi kuupiga mti uliokuwa karibu na banda walipojihifadhi wakati mvua ikinyesha.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita karibu na vituo viwili vya mabasi ya daladala na yaendayo mikoani kandokando ya Barabara ya Mbeya-Malawi.
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Chalya Nyangidu alisema tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana na kwamba aliyefariki dunia ni mkazi wa jijini Arusha, Freeman Swai (35) ambaye alifika mkoani hapa kununua ndizi.
Waliojeruhiwa na kupelekwa Hospitali ya Makandana ni Oliva Ipyana (45), Anna Jericho (30), Juliana Francis (32) na Stela Nsile (37) wakazi wa wilayani hapa.
Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk Marco Mbata alithibitisha kupokea mwili wa Swai na majeruhi wanne. Alisema baada ya uchunguzi ilibainika, Swai aliungua kwa moto wa radi na kusaidiana na simu iliyokuwa ikitumia kupiga muziki.

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Popular Posts

Our Facebook Page

Video